• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali Yatoa zaidi ya sh.Bilioni 1.7 kwa Halmashauri ya Mbeya Vijijini

Imetumwa : February 16th, 2018

Serikali imetoa zaidi ya shilingi Bilioni 1.7 kwaajili ya Ujenzi na ukarabati wa Vituo vya Afya vitatu katika Kata za Ilembo, Santilya na Ikukwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Mganga Mkuu wa Wilaya Dk Lausi Chomboka ameyasema hayo alipokuwa akitoa Taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Ilembo katika ziara ya Mkuu wa Mkoa kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho.

Dk Chomboka amesema kuwa fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa Maabara, Jengo la Upasuaji, wodi ya wazazi, wodi ya watoto, nyumba ya mtumishi, chumba cha kuhifadhia maiti, mfumo wa kukusanyia maji na sehemu ya kuchomea taka.

Amesema kuwa mradi wa ujenzi wa kituo cha afya Ilembo unagharimu Kiasi cha shilingi milioni 400 na ituo hicho cha afya kitahudumia vijiji 10 vyenye wakazi 17,166 kati hao, Wanawake 9,278 na wanaume 8,888 na kwamba Idadi ya wananwake wenye uwezo wa kushika mimba ni 3,777.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla amesema kuwa amekuja kujiridhisha namna Halmashauri na wananchi walivyojipanga kutumia fedha hizo zilizoletwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya

Mhe Makalla amewataka wananchi kushirika katika ujenzi wa kituo hicho mpaka kitakapokamilika bila kujali itikadi za siasa kwa kuwa wanatakaotumia kituo hicho ni watu wote  wa kata hiyo na amewaonya wanaopita kwa wananchi kuwashawishi kutoshiriki katika shughuli za miradi ya maendeleo.

Mhe Makalla ameagiza watumishi wa afya katika halmashauri na ofisi ya mkoa kuelekeza nguvu ya utendaji kazi katika ujenzi wa kituo cha afya Ilembo na ifikapo Mei 30 mradi ukamilike.

"Kuna watu wamekaa tu maofisini sasa ninaagiza kuanzia sasa waweke kambi huku ilembo ili kusukuma kasi ya ujenzi wa mradi huo na ujengwe kwa ubora wa hali ya juu ili jamii iweze kupata huduma bora za afya ya Msingi hususani upasuaji na kuacha kutembea umbali mrefu kufuata huduama za afya,” amesema


Naye Kaimu Mganga Mkuu, Dk.Yahya Msuya amesema katika mpango wa awamu ya kwanza ya utekelezaji wa ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya,kati ya vituo 44 katika halmashauri 82, Mkoa wa Mbeya ulipata Vituo viwili katika Halmashauri ya Rungwe Kituo cha Afya Ikuti na Halmashauri ya Kyela Kituo cha Afya Ipinda.


" Kutokana na kufanya vizuri katika ujenzi wa vituo vya afya Rungwe na Kyela katika awamu ya pili kati ya vituo vya afya 139 nchi nzima mkoa wa mbeya umepata vituo sita na katika hatua za awali tumeanza na vituo vya afya Ikukwa,Santilya na Ilembo ambavyo vitagharimu Sh bilioni 1.7,"amesema.



Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Matokeo ya Kidato cha Sita 2020 August 21, 2020
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2021 Mkoa wa Mbeya. December 18, 2020
  • Fomu za Maelekezo kwa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano 2021 Shule za Mkoa wa Mbeya (Joining Instructions) June 07, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC Homera atoa siku 14 Tarura kupata Mkandarasi Mpya

    February 23, 2023
  • WAZIRI DKT MABULA AZINDUA MPANGO KABAMBE WA JIJI LA MBEYA

    February 21, 2023
  • WATOTO 5,236 WAPANGIWA VYUO MBALIMBALI VYA UFUNDI MKOANI MBEYA

    February 06, 2023
  • "Wananchi Tushirikiane kutokomeza ukatili wa Kijinsia" Rc Homera

    December 02, 2022
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Tovuti ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Ajira

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Uzunguni Road

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025 2503034

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa