• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Hakuna Kuwaondoa Wapiga Debe - RC Chalamila

Imetumwa : August 25th, 2018

Na Nebart Msokwa, MBEYA

SERIKALI mkoani Mbeya, imetangaza kuwa haina mpango wa kuwaondoa wapiga debe kwenye vituo vyote vya mabasi mkoani humo na badala yake itaweka utaratibu mzuri wa kuitambua shughuli hiyo kuwa ajira rasmi kwa vijana.

Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, wakati alipokuwa anazungumza na wapigadebe, makondakta na madereva wa daladala katika kituo cha mabasi cha Nane Nane jijini Mbeya.

Chalamila alisema serikali inakusudia kurasimisha shughuli hiyo kwa kuandaa utaratibu wa kundi la vijana wanaofanya shughuli hiyo kutambuliwa, kuandaliwa sare maalumu na kuwa na vitambulisho kama ilivyo kwa madereva na makondakta.

Aliwataka vijana hao kuwa walinzi wa amani katika maeneo hayo ikiwa ni pamoja na kukomesha vitendo vya udokozi wa mali za abiria na kwamba wao ndio watakaokuwa wanawashughulikia wezi na waharifu wengine kwenye maeneo yao ya kazi.

“Kwa muda mrefu imekuwa ikitangazwa kuwa serikali ina mpango wa kuwaondoa wapiga debe kwenye vituo vyote vya mabasi hapa nchini, nimekuja kuwatangazia rasmi kuwa hakuna atakayewaondoa, hii ni ajira kama ajira zingine,” alisema Chalamila.

Alilitaka kundi hilo kuwa mstari wa mbele katika kusimamia na kufuata sheria ili waendelee kufanya kazi hiyo kwa amani na utulivu pamoja na kushirikiana na Jeshi la Polisi kusimamia amani.

Baadhi ya vijana wanaofanya shughuli hiyo, waliishukuru Serikali kwa uamuzi huo huku wakiziomba halmashauri kuboresha baadhi ya huduma kwenye maeneo yao ya kazi vikiwemo vyoo ili kulinda mazingira.

Mmoja wa wapiga debe hao, Michael Mwanjobe, ambaye anafanya kazi katika kituo cha nane nane alisema kuwa baadhi ya abiria na watumiaji wa kituo hicho huwa wanalazimika kujisaidia kwenye maeneo yasiyoruhusiwa kutokana na choo cha Jiji kilichopo kuchelewa kufunguliwa.

Mwanjobe alisema huduma hiyo ni mhimu katika eneo hilo lenye mkusanyiko mkubwa wa watu ili pamoja na kulinda mazingira lakini pia walinde afya za watu.

“Hapa kuna choo cha jiji lakini kinafunguliwa kwa kuchelewa, tunaomba hawa wenzetu waweke utaratibu mzuri ili huduma kwenye maeneo haya wanayoingiza fedha ziwe bora,” alisema Mwanjobe.

Aidha alipendekeza kuwa kila kituo cha daladala kiwe na sare kwa ajili ya wapiga debe zenye rangi tofauti na kituo kingine ili kuwatofautisha kwa ajili ya kuwatambua kirahisi wakati wa shughuli yoyote.

Nao baadhi ya wasafiri, waliomba wapiga debe hao kuwa na heshima kwenye kazi yao kwa madai kuwa baadhi yao ni wadokozi na hivyo huwafanya wasafiri kukosa amani wanapofika kwenye vituo hivyo.

Mmoja wa wasafiri hao, Betrice Kasendo, alisema mara nyingi wapiga debe huwa wanalazimisha kuwapokea wasafiri mizigo wakidai wanawasaidia lakini wakati mwingine wanatokomea nayo.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Matokeo ya Kidato cha Sita 2020 August 21, 2020
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2021 Mkoa wa Mbeya. December 18, 2020
  • Fomu za Maelekezo kwa Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Tano 2021 Shule za Mkoa wa Mbeya (Joining Instructions) June 07, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC Homera atoa siku 14 Tarura kupata Mkandarasi Mpya

    February 23, 2023
  • WAZIRI DKT MABULA AZINDUA MPANGO KABAMBE WA JIJI LA MBEYA

    February 21, 2023
  • WATOTO 5,236 WAPANGIWA VYUO MBALIMBALI VYA UFUNDI MKOANI MBEYA

    February 06, 2023
  • "Wananchi Tushirikiane kutokomeza ukatili wa Kijinsia" Rc Homera

    December 02, 2022
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Tovuti ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Ajira

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Uzunguni Road

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025 2503034

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa